BEKI WA SIMBA SC SHOMARI KAPOMBE ATANGAZA KUSTAAFU KUICHEZEA TAIFA STARS


Beki wa Club ya Simba SC Shomari Kapombe ameamua kutangaza rasmi kuwa ameandika barua ya kustaafu kuichezea timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars, licha ya kuwa umri wake bado unaruhusu kuendelea kuitumikia Taifa Stars.

Kapombe ametangaza kufikia hivyo baada ya kutathmini afya yake, kwani anadai Taifa Stars inahitaji wachezaji watakao kuwa fiti kwa asilimia 100 na upande wake haoni kama anaweza kujitoa kwa asilimia 100 kwa sababu amekuwa akikumbwa na majeraha, hivyo kaomba aendelee kuitumikia timu yake ya Simba SC ambayo haina mashindano mengi zaidi ya Ligi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527