WAZALISHAJI WA CHUMVI MKOANI TANGA WAJENGEWA UWEZO KUONGEZA UZALISHAJI BORA



 MENEJA wa Kiwanda cha Kuzalisha Chumvi cha Neelkanth Salt Ahmed Liemba akizungumza wakati wa mkutano huo kushoto ni Mwenyekit wa Chama cha Wazalishaji wa Chumvi mkoa wa Tanga Abdul Nuur

 Mwenyekit wa Chama cha Wazalishaji wa Chumvi mkoa wa Tanga Abdul Nuur akizungumza wakati wa mkutano huo kulia ni MENEJA wa Kiwanda cha Kuzalisha Chumvi cha  Neelkanth Salt Ahmed Liemba
 MKURUGENZI wa  Kiwanda cha Kuzalisha Chumvi cha  Neelkanth Salt Liemba akizungumza wakati wa mkutano huo kulia ni Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Tanga Zabibu Napacho kushoto Mwenyekit wa Chama cha Wazalishaji wa Chumvi mkoa wa Tanga Abdul Nuur
 Sehemu ya wachimbaji wa madini ya chumvi wakiwa kwenye mkutano huo


MENEJA wa Kiwanda cha Kuzalisha Chumvi  cha Neelkanth Salt Ahmed Liemba amesema kwamba wamelazimika kuwajengea uwezo wazalishaji wa ndani namna ya kuongeza uzalishaji bora ili malighafi wanazozalisha iweze kuwa na ubora ambao utakuwa na tija kubwa.

Ahmed aliyasema hayo wakati wa kikao cha kujadili changamoto za wazalishaji chumvi mkoani Tanga ambapo alisema kwamba licha ya kuwa hapa nchini kuna maeneo mengi makubwa ya uzalishaji wa malighafi hiyo lakini bado haina ubora ambao unahitajika kwenye viwanda vya ndani.

Alisema kwa kuliona hilo wao kama kiwanda wamelazimika kukutana na wazalishaji hao ili kuweza kuwapa maelekezo ni aina gani ya chumvi ambayo wanahitaji kwa sasa ili waweze kujipanga kuongeza uzalishaji huo ambapo pia walipatiwa elimu kutoka kwa wataalamu wa kiwanda hicho.

Meneja huyo alisema pia kwamba uwepo wa uhaba wa Chumvi yenye ubora nchini umesababiosha wenye viwanda kulazimika kuagiza malighafi hiyo kutoka nje ya nchi ili kuweza kukidhi mahitajio ya soko la ndani jambo ambalo wamelazimika kutumia gharama kubwa.

“Sisi kwenye kiwanda chetu kwa siku tunahitaji tani 300 za malighafi huku uzalishaji ukiwa ni tani 250 kwa siku huku zaidi ya tani 50 ikipotea kutokana na ubora duni wa malighafi hivyo mkutano huu utakuwa chachu kubwa ya kuweza kuondosha changamoto za namna hiyo “Alisema

Aidha alisema kwamba changamoto kubwa ilikuwa ni kwamba wazalishaji wengi hasa watanzania wanazalisha chumvi ambao haina ubora kutokana na kwamba hawana elimu licha ya kwamba Tanzania kuna maeneo mengi ya ukanda wa bahari hivi sasa wameamua kushirikiana nao ili kukuza sekta ya chumvi nchini.

Meneja huyo alisema kwamba malengo yao soko la Tanzania  ni kuweza kukamata soko la ndani na nje  ikiwemo kuendelea kutoa elimu ikiwa ni msisitiza wa Rais Dkr John Magufuli ya serikali ya viwanda hivyo wao kama wazawa wameamua kuingia kwenye sekta hiyo na wataweza.

Awali akizungumza Mwenyekit wa Chama cha Wazalishaji wa Chumvi mkoa wa Tanga Abdul Nuur-alisema kwamba lazima wachimbaji wawe wazi kulipa kodi zao zinavyotakiwa ili waweze kuonekana wanachangia kwa serikali kwani hilo ndilo jambo muhimu kwa ukuaji wa maendeleo.

Naye kwa upande wake Afisa Mkazi wa Madini mkoa wa Tanga Zabibu Napacho alisema ili wachimbaji wa chumvi wazalishe lazima waweze kukidhi vigezo vya uzalishaji huku akiwaeleza kwamba wao kama ofisi ya madini watakuwa tayari kutoa ushirikiano wa kutosha kwao wawekezaji ili waweze kuendeleza zao hilo la chumvi na madini hayo.

Hata hivyo alisema pia changamoto kubwa ni ukosekanaji wa masoko lakini wanaishukuru kampuni ya Neelkat kuja Tanga na kuwawezesha wachimbaji kupata soko la uhakika.

“Lakini naomba mapato ya serikali kila mmoja awe mfanyabiashara hai mwenye leseni ya uchimbaji wa madini ya chumvi…wale ambao hawana leseni wahakikishe wanakuwa nazo “Alisema

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527