RAIS MAGUFULI AWEKA MAWE YA MSINGI MIRADI YA UMEME, HOSPITALI YA WILAYA NA BARABARA YA MPANDA - IFUKUTWA - VIKONGE

Rais Magufuli jana Oktoba 11, 2019  amezindua mradi wa umeme wa Megawati 132 mkoani Katavi ambapo alisema mradi huo utaokoa zaidi ya Sh5.5 bilioni zilizokuwa zikitumika kununua mafuta kwa ajili ya majenereta ya kufua umeme.


Awali, Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani alisema mradi huo ulianza Mei 2019 na unatarajiwa kukamilika Mei 2020.

Alisema mradi huo utagharimu Sh135 bilioni na ulianza kwa  kujenga kituo cha kusambaza umeme kitakachofungwa mashine mbili za megawati 50 kila moja.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527