MWANDISHI ERICK KABENDERA ATAKA KUONGEA NA DPP ILI KUMALIZA KESI YAKE


Wakili Jebra Kambole  anayemtetea mwandishi wa habari nchini Tanzania, Erick Kabendera katika kesi namba 75/2019, jana ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi mwandamizi, Augustine Rwizile  kuwa wanakusudia kufanya majadiliano na ofisi ya Mwendesha mashtaka kuhusu tuhuma za uhujumu Uchumi zinazomkabili Mwandishi wa habari, Erick Kabendera.

Awali, wakili wa Serikali Wankyo Simon aliieleza  mahakama hiyo kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi bado haujakamilika. 

Alisema ni kweli jambo hilo lipo katika mchakato wa kuanza majadiliano na DPP, hivyo taratibu zikikamilika wataipa taarifa mahakama.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Octoba 24 itakapotajwa tena.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527