TUNDU LISSU ABADILI TAREHE YA KURUDI NCHINI


Aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu amesema hatarejea Tanzania Septemba 7, 2019 kama ilivyopangwa badala yake atasubiri ruhusa ya madaktari wanaomtibu.

Lissu ametoa kauli hiyo jana Jumanne Septemba 3, 2019 katika mahojiano na Shirika la Utangazaji Uingereza (BBC), alipoulizwa lini atarejea Tanzania.

Amesema  bado madaktari hawajaweka bayana kwamba atarudi lini.

"Nilisema mwanzoni nitarudi tarehe 7 Septemba, 2019 lakini daktari wangu ameniambia ataniona tarehe 1 Oktoba, 2019 na mara ya mwisho ataniona mara ya mwisho tarehe 8 Oktoba, 2019, kwa hiyo ile ratiba ya mwanzo haitawezekana, kwa sababu daktari wangu anataka kuniona." amesema Tundu Lissu

Lissu, amekuwa nje ya nchi tangu Septemba 7, 2017 aliposhambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 na watu wasiojulikana akiwa eneo la makazi yake Area D, Dodoma akitoka kuhudhuria vikao vya Bunge.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527