Shule ya Sekondari Old Tanga inateketea kwa moto ulioanza leo mchana Jumatano Septemba 18, 2019.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Edward Bukombe amesema chanzo cha moto huo ulioteketeza chumba cha mikutano na cha kuhifadhi vifaa bado hakijafahamika.
Kikosi cha Zimamoto tayari kiko eneo la tukio kuuzima moto huo.