ROSA REE AWAFUATA GHETTO KIDS UGANDA..AWASHIRIKISHA KWENYE NGOMA YAKE


Mwanamuziki Rapper wa Kike Kutoka Tanzania amefunguka na kusema kuwa yupo Uganda Kupanua Mziki wake Katika nchi hiyo kwa kuwashirikisha Wanamuziki wakubwa huko wakiwemo Watoto maarufu wacheza Dance wanaitwa Getto Kids.


Ghetto Kids kutoka Uganda wamepata umaarufu Dunia nzima baada ya kushirikishwa na Wanamuziki French Montana na Chriss Brown Katika ngoma zao wakionyesha uwezo mkubwa wa Kucheza ..

Rosa Ree amesema anampango wa kutoa ngoma ya kucheza ambayo ndani yake atacheza yeye pamoja na hao watoto wa Ghetto Kids,.

 Amesema kwa sasa wako katika mazoezi ya wimbo huo kwa ajili ya kushoot Video


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527