RAIS MAGUFULI :SERIKALI KUENDELEZA MAHUSIANO MAZURI KATI YAO NA MADHEHEBU YA DINI NCHINI


Rais wa Dkt John Magufuli amesema kwamba serikali ina kila sababu ya kuendeleza mahusiano mzuri kati yao na madhehabu ya dini nchini kwa sababu kazi wanayoifanya haina mbadala wake kwenye jamii.


Hayo aliyasema jana kwenye hotuba yake iliyotolewa na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati alipomwakilisha kwenye Jubilee ya miaka 25 Uaskofu wa Askofu wa Jimbo Katoliki la Tanga Anthony Banzi.

Jubilee hiyo ilikwenda sambamba na ibada iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Kadinali Mstaafu Policapy Pengo, Maaskofu, Mapadre, Masista na watawa,Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamini Mkapa na Mkewe wakiwemo pia viongozi wa serikali wa sasa na wastaafu

Alisema kwamba anaamini kwa pamoja wanaweza kujenga na kuendelea kuimarisha amani na umoja uliopo hapa nchini kwa wakishirikiana na  kuongeza kasi ya watawezesha watanzania kupata maendeleo.

“Baba Askofu sisi kama serikali tutatimiza wajibu wetu kutengeneza mazingira mazuri kwa madhehebu ya dini kutekeleza wajibu wake kwani uhuru wa kuabubdu uliopo nchini unaheshimuwa na kutekelezwa kwa vitendo.

Aidha alisema pia wataendelea kushirikiana na kusaidia na madhehebu ya dini kwenye upande wa shughuli zenu za huduma za kiuchumi na kijamii wanazofanya watafanya hivyo kwa kutambua mchango wao muhimu unaotolewa na huduma hizo kwa maendeleo ya nchi na ustawi wa watu wake.

“Maombi yangu kwamba msiwaruhudu watu waovu kutumia fursa hiyo muhimu…tunapopata taarifa za kutumika kinyume hatutasumbuka sana wakati wote viongozi wa dini na serikali wana jukumu la ulezi na kuhakikisha wananchi wanaishi kwa amani umoja upendo na mshikamano.

Waziri Ummy alisema kwamba licha ya utofauti za dini, kabila rangi au vyama Rais Dkt Magufuli anasema tofauti hizo hatuna budi kuishi nazo na wasiziache zikawa nyufa za uhasama ambao sio zitaligawa taifa bali linaweza kulimonyony’oa hata kanisa.

Aidha alisema kwamba matumaini ya waumini wa Jimbo Katiloki la Tanga na wananchi ni kwako Mhashamu Banzi na sio ya kiroho peke yake hivyo atambue kwamba wanayomatarajio chini ya uongozi wake kanisa katoliki linaweza kuendelea kutoa huduma huduma za kijamii kama walivyfanya huko nyuma.

“Wana tanga wanayo matumaini makubwa kwa sababu wanathamin i na kutambua manufaa makubwa yanayofanya kwenye harakati za kujilete maendeleo kutokana na kazi kubwa mnayoifanya kuwapa maendeleo kutokana na kazi kubwa”Alisema

Waziri Ummy alisema kwamba Rais Magufuli ataendelea kutambua na kuthamani mchango wa viongozi wa dini nchini hususani kwenye suala la kuliombea Taifa ili liendelea kuwa na amani na utulivu uliopo ili kuwawezesha wananchi kushiriki kwenye shughuli za kimaendeleo.
Hata hivyo alisema kwamba Serikali ya awamu ya tano itaendelea kuunga mkono juhudu za makanisa na viongozi wa dini kwenye kujenga amani ya nchi na kuleta ustawi wa Taifa ikiwemo kujenga masikilizano endelevu kati ya taasisi za dini na serikali.

“Niwaambie ndugu zangu maaskofu kwamba Rais Dkt Magufuli anasema ataendeleza ushirkiano uliopo kati ya serikali na Kanisa Katoliki pia kuunga mkono shughuli za kanisa kwenye kutoa huduma za jamii hususani elimu,afya na nyengine”Alisema.

Awali akitoa salamu za kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani ,Balozi wa Papa nchini Askofu Mkuu Marek Solczriski alisema kuwa mchango wa askofu Banzi ni mkubwa kwa kanisa na uhudumu wake wa kazi za kanisa umekuwa ni kichocheo cha maendeleo .

“Nakuombea katika kipindi hiki cha kusherehekea maadhimisho ya miaka 25 kiwe sababu za Baraka kwako na jimbo zima la Tanga na Mungu aendelee kukulinda na kukuongoza”alisema Mwakilishi huyo.

MWISHO


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527