POLISI KIGOMA WAUA WATUHUMIWA 12 WA UJAMBAZI WANAODAIWA KUTOKEA BURUNDI

Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma limefanikiwa kuwaua majambazi 12 katika majibizano ya risasi baina ya majambazi hao na Polisi usiku wa kuamkia jana katika eneo la mashamba ya kilemba kijiji cha Kalemba Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma.


Akizungumzia kijijini hapo jana Ijumaa Septemba 13, 2019 Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, Martin Otieno amesema siku za hivi karibuni kumeibuka matukio ya utekaji magari, baadhi ya waliokamatwa walieleza matukio hayo.

Amesema polisi walifika eneo hilo na kuanza kurushiana risasi na watu hao na kuwaua 12 waliokutwa na bunduki tatu aina ya AK 47, risasi 107, mapanga, visu na mabomu matatu ya kurusha kwa mkono.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527