MTALII AFARIKI AKIRUKA ANGANI NA PARACHUTI KUTOKA KILELE CHA MLIMA KILIMANJARO

Na Florah Temba na Fina Lyimo, Mwananchi

Justin Kyllo (51), raia wa Canada amekufa baada ya Parachuti alilokuwa akitumia kuruka angani kutoka kilele cha mlima Kilimanjaro nchini Tanzania kugoma kufunguka.

Akizungumza leo Jumamosi Septemba 28, 2019 kamishna msaidizi mwandamizi wa Hifadhi za Taifa (Tanapa), Pascal Shelutete amethibitisha kifo cha mtalii huyo, kwamba kimetokea katika kituo cha Stella Point kilichopo katika mlima huo.

Amesema mtalii huyo alifika Septemba 20, 2019 kwa ajili ya kupanda mlima, leo asubuhi alitumia Parachuti kwa ajili ya kuruka angani ili kushuka chini ya mlima lakini iligoma kufunguka na kusababisha kifo chake.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527