MCHUNGAJI AFARIKI AKIFUNGA SIKU 30 ....SIKU ALIBAKIZA 10



Mchungaji Brighton Samajomba kutoka nchini Zambia, amefariki dunia kwa kinachotajwa kupatwa na Utapiamlo' akiwa katika mfungo ambao alikuwa anadhamiria kufikisha siku 30.

Mpaka anafariki mchungaji huyo alikuwa amefikisha siku 20 hivyo zilikuwa zimebaki siku 10 tu kutimia siku 30, Kaka wa Marehemu Reagan Samajomba anasema ndugu yake alikuwa na kawaida ya kufunga na kufanya maombi kwa muda mrefu kuliko wengine.

Katika mfungo wa siku 30 Kaka wa Marehemu anasimulia kuwa ndugu yake aliamua kufanya hivyo huku lengo kuu likiwa kuiombea familia yake pamoja na waumini wa kanisa analoliongoza mshikamano pamoja na umoja uzidi kuimarika.

"Jambo jema alilotuachia sisi kama familia ni namna alivyofariki sababu alikuwa karibu na Mungu," alisema Kaka wa Marehemu.

Vyanzo: Zambia watchdog, Nairaland, Iharare.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527