Picha : ILANI YA UCHAGUZI YA WANAWAKE UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA NA UCHAGUZI MKUU TANZANIA 2020 YAZINDULIWA


Ilani ya Uchaguzi ya Wanawake ya Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2020 imezinduliwa rasmi leo Septemba 27,2019 wakati wa kufunga Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam.

Ilani hiyo inayojumuisha sauti za wanawake kutoka sauti za wanawake kutoka makundi mbalimbali chini ya Uongozi wa TGNP Mtandao kwa kushirikiana na Taasisi ya Women Fund Tanzania na Mtandao wa Wanawake na Katiba,Uchaguzi na Uongozi imezinduliwa na Mwenyekiti wa TGNP Mtandao Asseny Muro.

Awali akizungumza,Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanawake na Katiba,Ruth Meena alisema ilani hiyo imebeba masuala muhimu yanayohusu wanawake kwenye uchaguzi.

"Ilani hii imebeba ajenda ya mwanamke,turufu ya ushindi 2019/2020 imewalenga wanawake,serikali,vyama vya siasa,wagombea nafasi za uongozi,vyombo vya habari na wapiga kura",alisema Muro.

Alisema ilani hiyo inaendeleza madai ya wanawake watetezi wa haki za ushiriki katika uongozi wa kisiasa tangu taifa lipate uhuru mpaka leo.

"Hii ni ilani ya tano iliyobeba madai ya wanawake tukiwa wadau na washiriki wakuu katika michakato mbalimbali ya uchaguzi.Ilani ya kwanza ilikuwa ya mwaka 2000 ikijulikana kama ilani ya wapiga kura,ilani ya pili ni ya mwaka 2005,ya tatu ni ya mwaka 2015 na ya nne ni ilani ya mwaka 2015",alieleza Muro.

"Sisi wanawake wapiga kura tunatambua ni wadau muhimu kwenye shughuli zote za kisiasa na maendeleo ya jamii.Tunatambua na kudai haki za kushiriki katika uchaguzi kama wapiga kura na wanaowania nafasi za uongozi,walioteuliwa na kugombea hatimaye kushinda nafasi za uongozi kupitia uchaguzi",aliongeza.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao,Lilian Liundi alisema madai yaliyomo kwenye ilani ya uchaguzi ya wanawake yanahusu masuala ya wanawake wote nchini Tanzania.
Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanawake na Katiba,Ruth Meena akielezea kuhusu Ilani ya Uchaguzi ya Wanawake ya Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2020 ambayo imezinduliwa rasmi leo Septemba 27,2019 wakati wa kufunga Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam.
Kulia ni Mwenyekiti wa TGNP Mtandao Asseny Muro akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Ilani ya Uchaguzi ya Wanawake ya Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2020 
Mwenyekiti wa TGNP Mtandao Asseny Muro akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Ilani ya Uchaguzi ya Wanawake ya Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2020 
Mwenyekiti wa TGNP Mtandao Asseny Muro akionesha Ilani ya Uchaguzi ya Wanawake ya Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2020 
Mwenyekiti wa TGNP Mtandao Asseny Muro akionesha Ilani ya Uchaguzi ya Wanawake ya Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2020.
Wafanyakazi wa TGNP Mtandao wakionesha mabango yenye ujumbe wa 'Uongozi sio misuli ni hekima na busara kila mtu anao'.
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao Lilian Liundi akionesha Ilani ya Uchaguzi ya Wanawake ya Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2020 .
Mwenyekiti wa TGNP Mtandao Asseny Muro akimkabidhi Ilani ya Uchaguzi ya Wanawake ya Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2020,Mkurungezi wa Jinsia Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Julius Mbilinyi.
Uzinduzi wa Ilani ya Uchaguzi ya Wanawake ya Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2020 ukiendelea.

Uzinduzi wa Ilani ya Uchaguzi ya Wanawake ya Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2020 ukiendelea.
Wanaharakati wakisherehekea wakati wa uzinduzi wa Uzinduzi wa Ilani ya Uchaguzi ya Wanawake ya Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2020.

Wanaharakati wakisherehekea wakati wa uzinduzi wa Uzinduzi wa Ilani ya Uchaguzi ya Wanawake ya Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2020.
Wanaharakati wakisherehekea wakati wa uzinduzi wa Uzinduzi wa Ilani ya Uchaguzi ya Wanawake ya Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2020.
Wanaharakati wakisherehekea wakati wa uzinduzi wa Uzinduzi wa Ilani ya Uchaguzi ya Wanawake ya Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa Tanzania mwaka 2020.

Mkurungezi wa Jinsia Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Julius Mbilinyi akizungumza wakati wa kufunga Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam.

Mkurungezi wa Jinsia Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Julius Mbilinyi akizungumza wakati wa kufunga Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam.
Mkurungezi wa Jinsia Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Julius Mbilinyi akizungumza wakati wa kufunga Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Soma pia : TAMASHA LA 14 LA JINSIA LAFUNGULIWA JIJINI DAR ES SALAAM

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527