BUNGE LAFANYA AZIMIO LA KUMPONGEZA RAIS MAGUFULI KWA KUCHAGULIWA KUWA MWENYEKITI SADC

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Leo Sept.3,2019 limefanya azimio la kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli baada ya hivi Karibuni kupewa nafasi ya kuwa Mwenyekiti wa Bunge la Jumuiya Ya Madola  Afrika SADC.

 
Mwenyekiti  kamati ya Bunge ya Mambo ya nje  na Usalama  Mhe. Musa Azan Zungu amesema Waasisi wa Jumuiya ya maendeleo nchi wanachama wa Kusini Mwa Afrika wamefanya makubwa ikiwa ni pamoja na  kuunganisha nchi wanachama hivyo matamanio ya waasisi hao ikiwa ni pamoja na Rais wa awamu ya Kwanza Mwl.Julius Kambarage Nyerere na Aman Abeid Karume yanatimizwa na Rais Magufuli katika kusukuma mbele maendeleo .

Nao baadhi ya Wabunge wamesema kuchaguliwa kwa Rais Magufuli kuwa Mwenyekiti  wa SADC itasaidia kuondoa kuritimba wa masoko katika  biashara  huku  pia wakisema kuwa Tanzania ni Kitovu cha Cha Ukombozi kwa nchi wanachama wa SADC katika kupigania Uhuru.

Akihitimisha katika Azimio hilo la Pongezi  bungeni jijini Dodoma Mhe.Zungu amesema ili Nchi wanachama wa SADC kujikomboa lazima kwanza kutafuta masoko ya ndani



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527