BONANZA KUADHIMISHA MIAKA MITATU YA MISENYI JOGGING CLUB LAFANA..DC MWILA ATAKA WANANCHI WAFANYE MAZOEZI


Lydia Lugakila - Malunde 1 blog
Mkuu wa wilaya ya Misenyi mkoani Kagera Kanali Denice Mwila amewataka wananchi wilayani humo kuepuka kutumia gharama nyingi katika matibabu badala yake wajikinge na maradhi kwa kufanya mazoezi.

Kanali Mwila ametoa wito huo Septemba 28,2019 wakati wa Bonanza la kwanza la kuadhimisha miaka 3 ya Misenyi Jogging Club lililofanyika katika uwanja wa mashujaa Bunazi wilayani humo likiwa na lengo la kuwahamasisha wananchi kuipenda michezo ili kutekeleza agizo la Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan la kufanya mazoezi.

Kanali Denice Mwila amesema kuwa kupitia Bonanza hilo wananchi wanapaswa kujenga utamaduni wa kupima afya zao na kufanya mazoezi kwani michezo ni afya.


"Naomba tushirikiane kuhamasisha jamii kuwa na mwamuko wa kufanya mazoezi ili kufukuza magonjwa nyemelezi",amesema.

Kwa upande wake Mratibu wa Tamasha la Misenyi Jogging Respicius John amewapongeza wadau wote walioshiriki kikamilifu vikiwemo vyombo vya habari mkoani Kagera vilivyotangaza tamasha hilo bure kuanzia mwanzo mpaka linamalizika kuwaomba wananchi wilayani Misenyi kujitokeza kwa wingi katika kufanya mazoezi.

Respicius amesema malengo ya baadae ni kuhakikisha jamii inakuwa na nguvu kubwa katika mazoezi na kuwataka wazazi kuwaruhusu watoto wao kushiriki mazoezi ili kukuza na kuimalisha miili yao.

Bonanza hilo limeenda sanjari na utoaji wa huduma za upimaji afya ikiwemo upimaji wa VVU na kuchangia damu pamoja na michezo mbali mbali ikiwemo kuvuta kamba, kukimbia kwenye magunia kucheza Draft, pete, mpira, kumenya ndizi kwa wanaume mchezo ambao ulienda kiushindani kati ya timu zilizopewa majina ya Simba na Yanga.
Wanafunzi wa shule ya msingi Bunazi wilayani Misenyi wakionesha vipaji vyao wakati wa Bonanza la kwanza la kuadhimisha miaka 3 ya Misenyi Jogging Club lililofanyika katika uwanja wa mashujaa Bunazi wilayani humo.


 Mwanafunzi wa shule ya msingi Bunazi wilayani Misenyi akionesha kipaji chake.

Mkuu wa wilaya ya Misenyi Kanali Denice Mwila akiwa katika michezo pete

Mkuu wa wilaya ya Misenyi Kanali Denice Mwila akihamasisha wananchi kuipenda michezo.
Mratibu wa bonanza hilo Respicius John akizungumza wakati wa  bonanza.
Mchezo wa  kuvuta kamba ukiendelea

Mchezo  wa kushindana kumenya ndizi ukiendelea.
Mbio za magunia zikiendelea.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527