WALIOFARIKI AJALI YA LORI LA MAFUTA MOROGORO WAFIKA 97


Idadi ya waliofariki katika ajali ya Lori iliyotokea mkoani Morogoro imezidi kuongezeka na kufikia 97 baada ya majeruhi wawili kati ya 20 waliokuwa wamelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam kufarikii dunia.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano MNH, Aminiel Aligaesha amesema majeruhi waliobaki hospitalini hapo ni 18 ambao wote wapo kwenye chumba cha uangalizi maalum (ICU).

Amewataja waliofariki ni Rosijo Mollel (35) aliyefariki jana Jumapili mchana na Neema Chakachaka ambaye amefariki alfajiri ya leo Jumatatu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527