VYAMA 18 NA WAGOMBEA 60 WAJITOKEZA KUCHUKUA FOMU ZA UCHAGUZI MDOGO WA UDIWANI KATA 13


Tume ya Taifa ya Uchaguzi iliutangazia Umma kuhusu Uchaguzi Mdogowa Udiwani katika Kata 13 za Tanzania Bara utakaofanyika tarehe 17 Agosti mwaka 2019,kwa kuzingatia matakwa ya kifungu cha 13 (3) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa Sura Na. 292.

Kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi huo, Utoaji wa Fomu za wagombea ulipangwa kufanyika kuanzia tarehe 29 Julai hadi 03 Agosti, 2019 na Uteuzi wa wagombea kufanyi katarehe 03 Agosti, 2019.

Hadi kufikia tarehe 02 Agosti, 2019 saa 10:00 jioni jumla ya wagombea 60 kutoka vyama vya siasa 18 wamechukua fomu za uteuzi.

Vyama vilivyochukua fomu hadi sasa na idadi ya wagombea waliochukua fomu kwenye mabano ni Chama cha DEMOKRASIA MAKINI(5) AAFP (5), CCK(3), DP (4), SAU (4), UDP(4) ACT Wazalendo (3), UPDP (5), ADC (2), TLP (1), CCM (12), ADA TADEA (4), CHADEMA (2), CHAUMA (1), NRA (1), NLD (1), CUF (2)na UMD (1).
Imetolewa leo tarehe 02 Agosti, 2019 na
 Hussein Makame
AFISA HABARI
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527