RAIS MAGUFULI AMTUMBUA MKURUGENZI WA HALMASHAURI

Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Morogoro Vijijini, Kayombe Rioba kwa utendaji usioridhisha wa miradi ya maendeleo hususani ujenzi wa Hospitali ya Wilaya.


Uamuzi wa kuondolewa kwa kiongozi huyo umetangazwa na Waziri wa nchi ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Seleman Jafo leo.

"Leo tarehe moja mwezi wa 8 mwaka 2019, Mh. Rais Magufuli amemtengua Mkurugenzi wa Halashauri ya Wilaya ya Morogoro Bwn. Kayombe Masoud Rioba kutokana na usimamizi usioridhisha wa miradi ya maendeleo hususani ujenzi wa Hospitali ya Wilaya," amesema leo Waziri Jafo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527