TETESI ZA SOKA LEO IJUMAA AGOSTI 30,2019

Mchezaji wa kiungo cha kati wa Manchester United na timu ya taifa ya Ufaransa Paul Pogba, mwenye umri wa miaka 26, hatosaini kuongeza mkataba wake hivi sasa na anataka kujiunga na Real Madrid haraka iwezekanavyo. (Marca)

Paris St-Germain inamtaka kiungo wa kati wa Tottenham Christian Eriksen mwenye umri wa miaka 27, kama mchezaji atakayeichukua nafasi ya mchezaji wa timu ya taifa ya Brazil Neymar, anayekaribia kurudi Barcelona. (Le Parisien)

Bayer Leverkusen inataka kumsaini beki wa kati wa Tottenham na timu ya taifa ya Ubelgiji Jan Vertonghen, aliye na miaka 32, kabla ya kuwadia Jumatatu muda wa mwisho wa dirisha la uhamisho Ulaya. (Kicker)

Beki kamili wa Manchester United na timu ya taifa ya Italia Matteo Darmian, mwenye umri wa miaka 29, yupo katika majadiliano kurudi katika ligi ya Serie A na klabu ya Parma. (La Gazzetta dello Sport kupitia Football Italia)

Mchezaji wa kiungo cha kati wa Arsenal na timu ya taifa ya Misri Mohamed Elneny, aliye na miaka 27, yupo katika mazungumzo na timu ya Uturuki Besiktas kuhusu uhamisho wa msimu mzima kwa mkopo (Sky Sports)
Meneja wa Gunners Unai Emery anasema beki kamili mwenye umri wa miaka 33 Nacho Monreal, aliyehusishwa na uhamisho kwenda Real Sociedad, huenda akaondoka katika klabu hiyo kabla ya kufungwa kwa dirisha la uhamisho Ulaya. (Mirror)

Bosi wa Tottenham Mauricio Pochettino anasua sua kumuita mlinzi wa timu ya taifa ya Ivory Coast Serge Aurier kwa Derby ya London kaskazini siku ya Jumapili huko Arsenal wakati mchezaji huyo wa miaka 26 akiwa anaweza kuondoka kabla ya kufungwa dirisha la uhamisho Ulaya Jumatatu. (Evening Standard)

Manchester United ilijitoa katika mkataba wa msimu wa joto ya mshambuliaji wa Juventus Paulo Dybala, mwenye umri wa miaka 25, kutokana na matakwa ya malipo ya mchezaji huyo wa Argentina ya thamani ya £18m kwa mwaka. (Mail)

Aliyekuwa mshambuliaji wa Manchester United Romelu Lukaku, mwenye umri wa miaka 26, amepunguza uzito wa mwili baada ya kufuata muongozo wa lishe chini ya meneja Antonio Conte tangu raia huyo wa Ubelgiji kujiunga na Inter Milan. (Mail)

Mlinzi wa Barcelona Gerard Pique anatumai kuwa Harry Maguire ataweza kuisaidia klabu yake ya zamani Manchester United kushinda taji la ligi kuu ya England. (Express)
Mchezaji wa kiungo cha kati wa Aston Villa Aaron Tshibola amejiunga na timu ya Ubelgiji Waasland-Beveren kwa mkataba wa miaka mitatu. (Birmingham Mail)

Arsenal dhidi ya Tottenham inajitayarisha kuipiku Liverpool dhidi ya Everton katika mchezo mkali wa Derby katika ligi kuu ya England. (Sun)

Kipa wa Paris St-Germain Alphonse Areola, mwenye umri wa miaka 26, amekubali kujiunga na Real Madrid. (RMC Sport)

Mchezaji wa kiungo cha mbele wa Chile Alexis Sanchez, mwenye umri wa miaka 30, ametuma ujumbe kwa wachezaji wenzake wa Manchester United katika Instagram kabla ya kujiunga na Inter Milan kwa mkopo. (Manchester Evening News)
Meneja wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer yupo tayari kusubiri hadi msimu ujao w ajoto kushinikiza kiungo cha ushambilizi , huku mchezaji wa kiungo cha mbele wa Borussia Dortmund Jadon Sancho, mwenye umri wa miaka 19, akisalia kuwa mchezaji anayemlenga pakuu. (Evening Standard)

Barcelona na Paris St-Germain zimekubali malipo ya uhamisho wa mchezaji wa miaka 27 wa timu ya taifa ya Brazil Neymar, lakini majadiliano yanaendelea kuhusu makubaliano ya mkataba huo. PSG inataka mchezaji wa kiungo cha mbele wa Ufaransa Ousmane Dembele, mwenye umri wa miaka 22, kuwa sehemu ya mpangilio huo. (Mirror)

Hatahivyo, Ajenti wa Dembele anasema mchezaji huyo hatoondoka Nou Camp, hatua ambayo huenda ikachangia kupromoka kwa pendekezo la uhamisho wa Neymar kwenda Barcelona. (Daily Mail)

Mchezaji wa kiungo cha kati wa Chelsea raia wa Ufaransa Tiemoue Bakayoko, mwenye umri wa miaka 25, amekubali makubaliano ya kujiunga upya na Monaco kwa mkopo - huku kukipangiwa malipo ya £31.8m ka mkataba wa kudumu.(RMC Sport, kupitia Sun)
Mlinzi wa Arsenal Nacho Monreal, mwenye umri wa miaka 33, c huenda akarudi katika klabu alikotoka Uhispania kaba ya kufungwa dirisha la uhamisho Ulaya Jumatatu, huku Real Sociedad ikiwa na hamu kubwa ya kumsajili mchezaji huyo wa zamani wa Osasuna na Malaga. (Evening Standard)

Mshambuliaji wa Arsenal na timu ya taifa ya England Sam Greenwood, mwenye umri wa miaka 17, ametambuliwa na timu bingwa ya Italia AC Milan na Juventus kama mchezaji anayelengwa baada ya kuridhisha maajenti katika mshindano ya ubingwa wa Ulaya wa timu za wachezaji walio chini ya umri wamiaka 17 mapema msimu huu wa joto. (Sun)
Chanzo - BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527