TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAMOSI AGOSTI 3,2019

Kiungo wa kati wa kimataifa wa Ureno Bruno Fernandes, anayehusishwa na taarifa za kuhamia Tottenham na Manchester United, ameliambia gazeti la Sporting Lisbon kuwa anataka kuondoka kwenye klabu hiyo msimu huu . Sporting wanaamini atataka euro milioni 70 au pauni £64m kwa ajili ya nahodha huyo mwenye umri wa miaka 24 . (Record, via Mirror)

Manchester United wanasemekana kusaini mkataba na Fernandes baada ya kombe la Super Cup la Portugal . (Express)

Mshambuliaji wa Juventus na Argentina Paulo Dybala, mwenye umri wa miaka 25, anataka malipo ya pauni 350,000 kwa wiki ikiwa atajiunga na Manchester United. (Sun)Mshambuliaji wa Juventus na Argentina Paulo Dybala, mwenye umri wa miaka 25, anataka malipo ya pauni 350,000

Mlinzi wa zamani wa Liverpool Andrea Dossena, mwenye umri wa miaka 37, ambaye kwa sasa yuko na Piacenza, amemueleza mchezaji mwenzake katika timu ya Palermo Dybala, ni bora ahamie ahamie Anfield kuliko Manchester United. (Liverpool Echo)

Tottenham wanataka mchezaji mbadala wa kukaba nafasi iwapo watamuuza Christian Eriksen, mwenye umri wa miaka 27, baafda ya muda wa mwisho wa kipindi cha kuhama kwa wachezajii cha waingereza kukamilika Alhamisi. Klabu za Uhispania zina hadi Agosti 31 kusaini mkataba na wachezaji . Pamoja na Fernandes, Spurs wanafanya mazungumzo na Real Betis kwa ajili ya mchezaji wa kimataifa wa Argentina Giovani lo Celso, mwenye umri wa miaka 23. (London Evening Standard)

Arsenal wanatarajia kutoa ofa mpya kwa ajili ya kiungo wa kati- wa Celtic Kieran Tierney katika siku zijazo , baada ya kukataliwa dau mbili za awali kwa ajili ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Uskochi mwenye umri wa miaka 22 . (Sky Sports)

kiungo wa kati wa Chelsea na wa timu ya kimataifa ya Ufaransa N'Golo Kante, mwenye umri w amiaka 28, anasisitiza kuwa atakuwa Stamford Bridge msimu huu, licha ya taarifa zinazomuhusisha na Paris St-Germain. (Express)Tottenham wanataka mchezaji mbadala wa kukaba nafasi iwapo watamuuza Christian Eriksen

Hatimae Tottenham wako tayari kukamilisha mkataba wa kikanda wa pauni milioni 30 ili kusaini mkataba na wa muda mrefu na target Ryan Sessegnon mwenye umri wa miaka 19, anayetoka safu wa nyuma-kushoto ya Fulham. (Mail)

Kiungo wa kati wa Ajax m Donny van de Beek, mwenye umri wa miaka 22, amethibitisha kuwa Real Madrid wameonyesha nia kwake. (Goal)

Dau la Manchester City kwa ajili ya mchezaji wa safu ya ulinzi ya Juventus na Ureno Joao Cancelo, mwenye umri wa miaka 25, atakuwa Danilo na kuondoka klabu hiyo . Akiwa na umri wa miaka 28 mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil anaweza kujiunga na Wataliano. (Manchester Evening News)Dau la Manchester City kwa ajili ya mchezaji wa safu ya ulinzi ya Juventus na Ureno Joao Cancelo, mwenye umri wa miaka 25, atakuwa Danilo na kuondoka klabu hiyo

Brighton wanatumai kusaini mkataba na mchezaji wa Brentford wa thamani ya pauni milioni 20 kiwango alichopewa mshambuliaji wa Ufaransa Neal Maupay, mwenye umri wa miaka 22, ambaye pia anafuatiliwa kwa karibu na Sheffield United pamoja na Aston Villa. (London Evening Standard)

Florentin Pogba, mwenye umri wa miaka 28- anayechezea zaidi guu la kushoto katika timu ya kimataifa ya Guinea safu ya kati-nyuma kwa sasa anaangaliwa na MLS Atlanta United ambaye ana kaka yake anayechezea safu ya kati ya mashambulizi ya Manchester United Paul, amepewa nafasi katika timu ya ligi ya pili ya Uhispania Fuenlabrada. (AS)

Hull watapata faida ya pauni milioni £9.45 kutokana na mauzo ya mlinzi wake wa zamani Harry Maguire kutoka kwa Manchester City. The Tigers walikubali mkataba wa 15% juu ya faida ya uhamisho walipomuuza kijana huyo mwenye umri wa miaka 26 kwa Leicester in 2017. (Hull Daily Mail)Manchester City wamekataa dau la pauni milioni 72 kutoka kwa Bayern Munich kwa ajili ya mshambuliaji wa Leroy Sane raia wa Ujerumani, mwenye umri wa miaka 23. (Metro)Manchester City wamekataa dau la pauni milioni 72 kutoka kwa Bayern Munich kwa ajili ya mshambuliaji wa Leroy Sane

City wanataka walipwe pauni milioni 137 kwa mauzo ya Sane ikiwa hatakuwa na haja ya kusaini mkataba wa kurefusha mkataba wake, unaomalizika Juni 2021. (Telegraph)

Mlizi wa England Harry Maguire, mwenye umri wa miaka 26, ameachwa nje ya kikosi cha Leicester kitakachocheza mechi ya urafiki baina yao na Atalanta Ijumaa kutokana na hali ya sintohfahamu juu ya hali ya yake ya baadae na Foxes wanaotaka mkataba wa pauni milioni 90 ikiwa Manchester United wanasaini mkataba nae. (Telegraph)
Dau la sasa la Manchester United kwa ajili ya Maguire ni la thamani ya pauni milioni 80

Dau la sasa la Manchester United kwa ajili ya Maguire ni la thamani ya pauni milioni 80 na klabu hiyo inaweza kutumia zaidi ya pauni milioni 150 kwa ujumla kabla ya kipindi cha mwisho cha mchakato wa uhamisho kukamilika (Independent)

Manchester United ilikataa fursa ya kusaini mkataba na mshambuliaji wa Juventus mwenye umri wa miaka 19 Moise Kean, na kumruhusu mtaliano huyo kuwa huru kuhamia Everton. (90min).
Chanzo - BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527