MBUNGE WA CHADEMA JOSEPH MBILINYI 'SUGU' AFUNGA NDOA



Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi maarufu Sugu leo Jumamosi Agosti 31, 2019 amefunga ndoa na Happiness Msonga katika Kanisa Katoliki Ruanda jijini Mbeya.
Katika misa hiyo wabunge 10 wa Chadema walihudhuria wakiongozwa na Meya wa Jiji la Mbeya, Mchungaji David Silinde.

Wabunge hao ni Frank Mwakajoka (Tunduma); Anthony Komu (Moshi Vijijini); Lucia Mlowe, Sophia Mwakagenda na Lucy Mollel (wote Viti Maalum).

Wengine ni Joseph Haule (Mikumi); Joseph Selasini (Rombo); David Silinde (Momba); Pascal Haonga (Mbozi) na Wilfred Lwakatare (Bukoba Mjini).

Viongozi wa Chadema walioshiriki misa hiyo ni mwenyekiti wa chama hicho Kanda ya Nyasa, Sadick Malila na katibu wake, Emmanuel Masonga.

Soma zaidi <<HAPA>>
Na Godfrey Kahango, Mwananchi 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527