MSHINDI WA SHINDANO LA MISS TANZANIA KUONDOKA NA MILIONI 10 LEO


Mrembo atakayeshikilia taji la Miss Tanzania 2019, anatarajiwa kupatikana leo katika kilele cha mashindano hayo katika ukumbi wa Millenium Tower, Makumbusho, Dar es Salaam.

Shindano hilo linawakutanisha warembo 20 kutoka kanda sita ambazo ni Nyanda za Juu Kusini, Kati, Mashariki, Ziwa, Dar es Salaam na Vyuo Vikuu.

Katika upande wa zawadi, mshindi atapewa shilingi 10,000,000.

Majaji wa shindano hilo ni Angela Damas (Miss Tanzania 2002), Shyrose Banji, Kenned The Remedy (Mtangazaji),  Miriam Ikoa na David Minja.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527