RAIS WA VENEZUELA ASEMA YUPO KWENYE MAZUNGUMZO NA DONALD TRUMP

Raisi wa Venezuela Nicolás Maduro amesema yupo kwenye mazungumzo na utawala wa raisi Donald Trump kwa miezi kadhaa sasa - licha ya vikwazo vipya vya Marekani kwa taifa hilo.

Mgogoro unaoedelea wa kisiasa na kiuchumi umeianya Venezuela kuwa na marais wawili waliojitangazia uhalali wa kuongoza.

Marekani ni moja ya mataifa 50 ambayo hayamtambui Maduro kama raisi halali wa Venezuela.

Utawala wa Washington ulitangaza vikwazo vipya dhidi ya Venezuela mwanzoni mwa mwezi kama njia ya kumuongezea Maduro shinikizo la kung'atuka.

Hata hivyo jana Jumanne, Maduro amethibitisha kuwa amekuwa kwenye mazungumzo na maafisa waandamizi wa serikali ya Trump kwa miezi kadhaa sasa.

Akizungumza kupitia runinga, Maduro amesema: "Kama nilivyofanya mazungumzo ndani ya Venezuela, pia nimetafuta namna ya kumfanya raisi Trump aisikilize Venezuela."

Raisi Trump pia amethibitisha kuwa utawala wake umekuwa kwenye "mazungumzo na wawakilishi wa Venezuela".

"Sitaki kusema nani, lakini tunazungumza na watu wa ngazi ya juu kabisa," amesema Trump.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527