KUNDI LA WAASI LA HOUTHI LA YEMEN LARUSHA MAKOMBORA 10 DHIDI YA UWANJA WA NDEGE WA SAUDI ARABIA

Kundi la waasi la Houthi la Yemen limesema lilirusha makombora 10 dhidi ya uwanja wa ndege wa Jizan nchini Saudi Arabia jana usiku.


Taarifa iliyotolewa na mtandao wa kituo cha televisheni cha al-Masirah kinachomilikiwa na kundi hilo imemnukuu msemaji wa jeshi la waasi hao Yahya Sarea akisema, makombora 10 aina ya Badr-1 yamerushwa kwa pamoja dhidi ya uwanja wa ndege wa Jizan, na yamelenga ndege za kijeshi na helikopta za kivita aina ya Apache ndani ya uwanja huo, na kwamba askari kadhaa wa Saudia wameuawa kwenye shambulizi hilo.

Pia amesema, jeshi la Houthi litafanya mashambulizi mengi zaidi katika kipindi kijacho.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527