WAKAMATWA KWA KUUZA JUISI YA TENDE YENYE 'NGUVU ZA KIUME AINA YA 4G'


Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi Zanzibar (ZFDA), imewakamata watu wawili kwa tuhuma za kuuza juisi ya tende iliyochanganywa na dawa ya kuongeza nguvu za kiume, kitendo kilichoelezwa kuwa si cha kibinadamu kwani dawa hizo huwa zinatolewa kwa utaratibu maalumu.


Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi wa ZFDA Nassir Buheti, ambapo ameyataja maeneo ambayo juice hiyo ilikuwa ikiuzwa kuwa ni Fuoni, Kiembesamaki, Mwanakwerekwe na Magari ya Mawe, na kuwataja watuhumiwa hao kuwa ni Hamid Salum na Hemed Salum, ambao wamekuwa wakiuza juice hiyo kwa watu mbalimbali.

"Walichofanya ni jambo la hatari kwa afya ya binadamu, lengo lao ni kuwavutia watu kuongeza nguvu za kiume, kumbe wanachanganya na dawa hizi wanaziita '4G kifurushi cha wiki', pia hawana kibali kwa upande wa chakula. Na aina ya dawa wanazoziuza zinatakiwa kutolewa kwa cheti maalumu," amesema Buheti.

Kwa upande wa watuhumiwa hao wamekiri kuchanganya juice ya tende na dawa ya kuongeza nguvu za kiume aina ya 4G - Viagra, ambayo walikuwa wakizinunua kwenye maduka ya dawa kwa lengo la kuwavutia wanaume na walikuwa wakisambaza juice hiyo kwa kutumia gari aina ya Spacio.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527