MAAFISA ARDHI 183 WASIMAMISHWA KAZI,MAJINA YAO YAMEPELEKWA TAKUKURU KWA UCHUNGUZI

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi ameelekeza kusimamishwa kazi kwa watumishi 183 kuanzia leo Agosti 7,2019 kupisha uchunguzi wa tuhuma za kuingilia mfumo wa kukadiria na kukusanya kodi ya pango a aradhi kinyume na taratibu na kusababisha upotevu wa mapato ya serikali.


Amemwelekeza katibu mkuu wa Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwasilisha orodha hiyo ya majina kwa mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU leo ili uchunguzi uanze mara mara moja


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527