WAZUNGU WATATU WALIOKAMATWA NA MADINI YA DHAHABU WARUDISHWA RUMANDE


Watu watatu raia wa kigeni kutoka nchi za Ireland na Uingereza wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya kwa tuhuma za kupatikana na madini aina ya dhahabu yenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 98 kinyume na sheria na taratibu za nchi.

Akisoma Shtaka Mwendesha Mashitaka wakili Msomi wa Serikali Mwandamizi Jacqueline Nyantori, anasema washtakiwa hao kwa pamoja wametenda kosa hilo la uhujumu uchumi July 3, 2019 na kukamatwa katika uwanja wa Ndege  Songwe uliopo Mkoani Mbeya ambapo walikutwa na madini aina ya yenye uzito wa gram 1043.33 yenye thamani ya shilingi milioni 98.5 .

Wakili huyo amewataja washtakiwa hao kuwa ni Clive Rooney (62) raia wa Irish ambaye ni Meneja wa fedha, Ross Harris (34) na Robert Wheedon (59)ambao ni raia wa Uingereza ambapo wamekamatwa na madini hayo wakiyasafirisha kuelekea Jijini Dar es Salaam.

Mwendesha mashtaka wa Serikali amesema washtakiwa hao wamekamatwa na Madini kinyume cha Sheria ya Uhujumu uchumi namba 18 (1) na 4 kifungu cha (1a) na kifungu cha sheria ya madini namba 14 cha mwaka 2010, ikiwa ni pamoja na aya ya 27 ya jedwali la kwanza na kifungu namba 57 kifungu kidogo.

Aidha Kaimu Hakimu Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya Venance Mulingi amesema Mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza shtaka hili ambapo washtakiwa wamerudishwa wamerudishwe rumande hadi July 22 mwaka huu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527