TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATANO


Manchester United wana nia kusaini mkataba na kiungo wa kati- nyuma wa Barcelona na Ufaransa Samuel Umtiti

Manchester United wana nia kusaini mkataba na kiungo wa kati- nyuma wa Barcelona na Ufaransa Samuel Umtiti, mwenye umri wa miaka 25. (Le10 Sport )

Paris St-Germain wameweka turufu yao ya uhamisho wa mshambuliaji wao Neymar mwenye umri wa miaka 27 kwa Barcelona. (Marca)

Arsenal wanakamilisha mkataba kwa ajili ya mchezaji wa safu ya kushoto-nyumba wa Celtic na Uskochi Kieran Tierney, mwenye umri wa miaka 22. (Mail)Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionParis St-Germain wameweka turufu yao ya uhamisho wa mshambuliaji wao Neymar kwa Barcelona

Kiungo wa safu ya mashambulizi wa Inter Milan na Argentina Mauro Icardi, mwenye umri wa miaka 26, anaweza kuwa anaelekea Napoli kwa mkataba wa euro milioni 80 (£73m) . (Corriere dello Sport - in Italian)

Crystal Palace wameweka dau la takriban pauni milioni 14 kwa ajili ya mshambuliaji wa timu za CSKA Moscow na Urusi -Fedor Chalov mwenye umri wa miaka 21 . (Sky Sports)

Mkurugenzi mkuu wa Bayern Munich Karl-Heinz Rummenigge anasema hakuelewa ni kwanini meneja Niko Kovac alisema kuwa klabu hiyo inaamini itasaini mkataba na winga Mjerumani Leroy Sane ambaye anaichezea sasa Manchester City akiwa na umri wa miaka 23. (Bild - in German)Mauro Icardi, mwenye umri wa miaka 26, anaweza kuwa anaelekea Napoli

Kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane anasema kuwa hafahamu ikiwa kiungo wa kati wa mashambulizi wa timu ya Colombia -James Rodriguez mwenye umri wa miaka 28 atakuwa kwenye klabu hiyo msimu ujao. (Marca)

West Brom hawajapokea ofa yoyote kutoka kwa Aston Villa kwa ajili ya winga wa uskochi Matt Phillips, mwenye umri wa miaka 28. (Birmingham Mail)

Mlindalango wa Newcastle na England wa kikosi cha walio chini ya umri wa miaka -21 Freddie Woodman,ambaye ana umri wa miaka 22, analengwa na Celtic na Arsenal, pamoja na klabu ambazo hazijatajwa za Championi. (Chronicle)Kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane anasema kuwa hafahamu ikiwa James Rodriguez atakuwa kwenye klabu hiyo msimu ujao

Newcastle wamekataliwa dau la pauni milioni 4.5 kwa jili ya kiungo wa kulia nyuma wa Amiens na Sweden Emil Krafth mwenye umri wa miaka 24 . (Sun)

Mchezaji wa klabu ya Partizan ya Serbia anayecheza safu ya kati-nyuma Strahinja Pavlovic, mwenye umri wa miaka 18, "ameshangazwa " na tetesi zinazomuhusisha na kuhamia Celtic. (Daily Record)Freddie Woodman , analengwa na Celtic na Arsenal

Meneja wa zamani wa Chelsea na Manchester United Jose Mourinho atarejea katika utawala wakati fursa itakapojitokeza. (Sky Sports)

Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United Teddy Sheringham anasema Ole Gunnar Solskjaer anapaswa kumuuza kiungo wa kati Mfaransa Paul Pogba mwenye umri wa miaka 26. (Talksport)Jose Mourinho atarejea katika utawala fursa itakapojitokeza

Kiungo wa kati wa Atletico Madrid Koke anasema kuwa anaamini mshambuliaji wa Ureno Joao Felix mwenye umri wa miaka 19-atakuwa "mmoja wa wachezaji bora zaidi duniani . (ESPN)

Preston North End wamekatalia mbali dau la deni kutoka kwa Wigan Athletic kwa ajili ya kiungo wa kati Daniel Johnson mwenye umri wa miaka 26-mzaliwa wa Jamaica. (Lancashire Evening Post)

CHANZO.BBC SWAHILI

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527