TECNO NA TIGO WATAMBULISHA RASMI PHANTOM 9


Dar es Salaam, Tanzania, 25/7/2019- Kampuni  maarufu ya simu nchini TECNO ikishirikiana na TIGO imezindua rasmi simu yao kubwa ya  TECNO Phantom 9 ikiwa ni mwendelezo katika matoleo ya Phantom ikiambatanishwa na ofa ya GB 18. TECNO Phantom 9 ni simu ya kwanza katika upande wa TECNO Phantom series kuja na kamera tatu za teknolojia ya AI (AI triple)  zenye 16MP+8MP+2MP. 


Akizungumza na vyombo vya habari Meneja  wa Uhusiano wa kampuni ya TECNO, Bwana Eric Mkomoye alisema kwamba “Katika ulimwengu wa sasa wa smartphone, kamera  zinapata ushindani mkubwa toka kwa kamera za simu  kwani kila mpiga picha  anatambua umuhimu wa kutumia simu yenye kupiga picha vizuri ili kuepuka usumbufu wa kujibebesha mizigo, na TECNO tumelifanyia kazi kupitia Phantom 9 kwani ina kila sifa zenye kukidhi haja ya wateja wetu  wanaopenda kuchukua matukio kupitia kamera za simu zao. 

Bwana Mkomoye aliongeza, “TECNO phantom 9 ikiwa kama “flag ship” ya kampuni kwa mwaka huu, TECNO imehakikisha ujuzi si katika upande wa kamera tu bali hata uwezo wa kuhifadhi files na speed ni mkubwa ikipewa uwezo na memory yenye GB 128Rom + 6Ram pamoja na Operating system ya Android Pie (P). lakini vile vile phantom 9 ina AMOLED Screen ya nch 6.4 FHD yenye kupiga picha  zenye rangi halisi na upana zaidi”.

Katika uzinduzi huo, Meneja Mawasiliano wa TIGO Tanzania, Bi. Woinde Shisael alizungumza machache kuhusiana na ushirika uliopo baina ya kampuni hizo mbili na namna ambavyo wateja wa Tigo watakaonunua simu hii ya Phantom 9 katika maduka ya Tigo au katika maduka ya wabia wetu watakavyonufaika na ofa ya mpaka GB 96 kutoka TIGO.

“TECNO na TIGO tukiwa kampuni pendwa na zenye kujali wateja wetu  tunafahamu ni kwa namna gani wateja wetu wanatamani kwenda sambamba na mfumo wa maisha ya kidigital na kwa kuzingatia hilo tumeileta rasmi Phantom 9  ikiwa na ofa ya mpaka  GB 98 kwa mwaka mzima ili wateja wetu waendelee kufurahia mtandao bora wakiperuzi mitandaoni”.  

Wateja wote wanaotaka kununua Phantom 9 wanaweza kuweka oda za awali (pre-order) katika maduka ya TECNO smart hubs yaliyoko Dar es salaam ,mtaa wa samora, kariakoo katika jingo la china plaza na pia mlimani city, kiasi cha shilingi 50,000 kitapokelewa na  siku ya kuja kuchukua simu mteja atamalizia pamoja  na kupewa zawadi maalumu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527