BENKI YA MAENDELEO YA WAKULIMA TADB YAJA NA NEEMA KWA WAKULIMA MKOANI KAGERA


Kaimu Meneja wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo TADB Kanda ya ziwa, Izirahabi Jumanne akizungumza wakati akizindua kampeni ya kuhamasisha wakulima kutumia mfumo rasmi wa kibenki

Na Lydia Lukagila - Malunde1 blog Kagera

Wakulima mkoani Kagera walio katika mazao ya mikakati wametakiwa kufuata agizo la Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Kassim Majaliwa la kupitia mifumo rasmi ya kibenki ili kukopesheka kwa urahisi.

Rai hiyo imetolewa  leo Julai 19 ,2019 na Kaimu Meneja wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo TADB Kanda ya ziwa, Izirahabi Jumanne wakati akizindua kampeni ya kuhamasisha wakulima kutumia mfumo rasmi wa kibenki na kufungua akaunti zao ili kupata fursa mbalimbali zitakazo wawezesha kukopesheka kwa urahisi katika ofisi ya Chama cha Ushirika mkoani Kagera.

Jumanne amesema Waziri Kassim Majaliwa alitoa agizo kwa wakulima wote walio katika mazao ya mkakati kupitia mifumo rasmi ya kibenki ili kuwawezesha wakulima hao kupata fursa mbali mbali za mikopo itolewayo na Benki ya Kilimo.

Amesema huu ni msimu wa pili wa kuhamasisha wakulima kutumia mfumo jumuishi kwani msimu wa kwanza ulifanyika mwaka 2018 japo changamoto kubwa ilikuwa ni elimu jambo ambao lilisababisha wakulima wengi kupata pesa zao kwa kuchelewa.

"Mfumo huu una malengo mahsusi, kwani mkulima atakopesheka wa haraka na kupata fursa mbali mbali za mikopo kwa urahisi ikilinganisha na aliyezunguka kupitia ofisi za vyama vya ushirika",amesema.

Naye Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoani Kagera Robert Kitambo amesema mfumo wa kulipia kupitia akaunti unampunguzia adha mpokeaji pesa na kutoa pesa anavyotaka tena kwa siri na kuepuka kusuala ya wavamizi.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Vodacom kutoka Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera Muda Tito amewahimiza wakulima kutunza pesa zao kupitia simu za mkononi na kuwa na kumbukumbu za namba zao za siri kwani inakuwa ngumu pale mkulima anaposahau namba za siri.

Tito ameongeza kuwa kuhusu masuala yoyote yatakayoleta ugumu wakulima waonane na makarani ili kumaliza matatizo yao.

Ikumbukwe kuwa kampeni hii ya kuhamasisha wakulima kutumia mfumo wa kulipia kupitia akaunti itafanyika katika wilaya zote za mkoa wa Kagera ili kuwasaidia wakulima kukopesheka kwa urahisi na kupata fulsa mbali mbali za mikopo ili kujikwamua kiuchumi.
Kaimu Meneja wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo TADB Kanda ya ziwa, Izirahabi Jumanne akizungumza wakati akizindua kampeni ya kuhamasisha wakulima kutumia mfumo rasmi wa kibenki. Picha zote na Lydia Lugakila - Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527