RAIA WA HUNGARY AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUKUTWA NA DAWA ZA KULEVYA

Raia wa Hungary Akos Berger (28), amepandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashitaka ya kusafirisha dawa za kulevya zenye uzito wa gramu  250  aina ya Amphetamine.


Berger amefikishwa mahakamani hapo  Juali 25,2019 na kusomewa mashitaka mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Maira Kasonde.

Akisoma hati ya mashtaka, Wakili wa Serikali, Grory Mwenda amedai,  Julai 19 mwaka huu, eneo la Mbezi Beach jijini Dar es Salaam, mshtakiwa alitenda kosa hilo.

Hata hivyo, baada ya kusomewa mashitaka hayo, Hakimu  Kasonde alimtaka mshitakiwa kutojibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi ya dawa za kulevya, isipokuwa kwa kibali maalumu kutoka kwa DPP

Upande wa mashitaka ulidai upelelezi wa kesi hiyo haujakamilka na kesi iliahirishwa hadi Agosti 9 mwaka huu itakapotajwa.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527