MBOWE AZUIWA KUFANYA MIKUTANO KUMPISHA DC SABAYA


Jeshi la Polisi Wilaya wa Hai limemtaka Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe kusitisha mikutano aliyopanga kuifanya kwa sababu DC Lengai Ole Sabaya anafanya ziara, hivyo mikutano itaingiliana, jambo linaloweza kusababisha uvunjifu wa amani.


 Ziara hiyo ya Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema ilitakiwa ianze leo lakini iliahirishwa jana Jumapili Julia 28, 2019 baada ya mbunge huyo kufiwa na kaka yake, Meja Jenerali Alfredy Mbowe.

Leo Jumatatu Julai 29, 2019 barua iliyotolewa na Mkuu wa Polisi wilayani ya Hai, Lwelwe  Mpina yenye kumbukumbu namba MB/JH/27/07/2019  kwenda kwa katibu wa mbunge (Mbowe) imezungumzia kusitishwa kwa ziara hizo za Mbowe.

Zuio hilo litakoma DC akimaliza ziara yake; “Kwa busara, sitisha ziara na mikutano unayotegemea kuifanya  hadi mkuu wa wilaya atakapomaliza ziara yake,” inasomeka barua hiyo


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527