JAMES MBATIA ACHAGULIWA TENA KUWA MWENYEKITI WA CHAMA CHA NCCR-MAGEUZI


James Mbatia amechaguliwa tena kuwa mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi kwa kipindi cha miaka mitano katika mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Akizungumza Jumapili Julai 28, 2019 mkuu wa oganaizesheni na utawala wa chama hicho  Florian Mbeo amesema mbali na Mbatia, pia umefanyika uchaguzi wa makamu mwenyekiti Bara na Zanzibar pamoja na wajumbe wa halmashauri kuu.

"Kwa mujibu wa katiba  ya chama chetu ikitokea nafasi mgombea akawa mmoja huwa tunapiga kura za ndio na hapana,” amesema Mbeo akizungumzia uchaguzi huo ambapo nafasi nyingi mgombea alikuwa mmoja.

Amesema nafasi ya mwenyekiti iliwaniwa na Mbatia pekee na kuibuka na ushindi kwa kura 210 za ndio na tisa za hapana.

Mbeo amesema nafasi ya makamu mwenyekiti bara iliwaniwa na Angelina John aliyepata kura 200 za ndio na 19 za hapana.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527