AGRA KUIMWAGIA MAMILIONI TANZANIA KATIKA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA PILI WA MAENDELEO YA SEKTA YA KILIMO [ASDP II]


Na.Faustine  Gimu Galafoni ,Dodoma.
Serikali ya Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania inatarajia kupokea zaidi ya Ya  Dola za Marekani laki sita kutoka Taasisi ya Mapinduzi ya kijani Barani Afrika ( Alience Green Revelotion in Afrika   AGRA)  Katika utekelezaji wa mradi wa mpango wa Maendeleo  ya  sekta ya kilimo  awamu ya pili[ASDP  II]. 


Hayo yamesemwa Julai 29,2019  jijini Dodoma  na Katibu Mkuu ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Mhandisi . Joseph Nyamhanga wakati akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kikao kazi cha Ofisi ya TAMISEMI ,Wizara ya Kilimo pamoja na AGRA Kilicholenga mpango mkakati wa maendeleo ya sekta ya kilimo awamu  ya pili[ASDP II  ambapo  amesema kuwa  kuna hatua kadhaa zitafanywa kabla ya kusaini mkataba huo ikiwa ni pamoja na kupata maoni ya Mwanasheria mkuu wa serikali na kuwasiliana na wizara ya fedha na mipango.

Hivyo,Mhandisi Nyamhanga amesema mradi huo utashirikikisha ngazi mbalimbali za Utawala ikiwa ni pamoja na  vijiji,kata,halmashauri,mikoa huku pia akisema  kuwa fedha hizo  ofisi ya TAMISEMI itasimamia ipasavyo kupitia maafisa kilimo na uongozi serikali za  mitaa. 


Naibu katibu mkuu Wizara ya kilimo Siza Donald Tumbo amesema kuwa mpango wa pili wa maendeleo ya kilimo lengo lake kuu  ni kuongeza uzalishaji pamoja na  kuondoa udumavu  na kuondoa dhana ya kilimo kwa ajili ya kuhimili njaa peke yake bali ni kujikita katika kilimo biashara. 


Malengo mengine ya ASDP II ni kuhakikisha upatikanaji wa pembejeo bora za kilimo kwa bei rahisi huku akibainisha kuwa changamoto ya usafirishaji wa Mazao kwa sasa haipo kwani miundo mbinu ya barabara iko vizuri na kilichobaki ni kuzalisha mazao bora  na upatikanaji wa masoko kwa urahisi zaidi.

Vianey Luendela ambaye ni  Meneja wa AGRA Nchini Tanzania amesema  AGRA imekuwa mdau wa maendeleo ya kilimo kwa miaka 15 nchini Tanzania na AGRA imesha wekeza  Dola Milioni 60 za Tanzania toka imeanzishwa katika eneo la kilimo.

Ikumbukwe kuwa ASDP ni mchakato wa muda mrefu uliobuniwa kutekeleza (ASDS), na ndiyo nyenzo kuu (main tool) ya Serikali katika kuratibu na kufuatilia maendeleo ya kilimo ambapo Programu hii inaoanisha utekelezaji kati ya wizara za sekta ya kilimo na wadau wengine na kuleta ufanisi katika mfumo wa usimamizi.  


Aidha, ASDP inaunganisha mahitaji halisi shambani katika ngazi ya wilaya na kuoanisha ufuatiliaji na uimarishaji wa uwekezaji katika ngazi ya kitaifa na kimataifa katika sekta ya kilimo huku Mtazamo mkuu wa ASDS na ASDP ni kuwapa uwezo wazalishaji wadogo, wa kati na wakubwa wa sekta ya kilimo kupata faida kutokana na kuongeza uzalishaji na tija katika shughuli zao. 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527