WIZARA YA AFYA KENYA YASEMA KUWA HAKUNA EBOLA

Matokeo ya utafiti wa damu ya mgonjwa aliyeshukiwa kuwa na virusi vya Ebola yameonyesha kwamba hana virusi vya ugonjwa huo.




Katika taarifa rasmi kwa vyombo vya habari, wizara ya afya nchini Kenya imetoa hakikisho kwamba hakuna kisa chochote cha Ebola nchini Kenya.

Waziri wa afya nchini Sicily Kariuki awali alijaribu kutuliza wasiwasi uliopo kwa kueleza kwamba dalili za mgonjwa aliyeshukiwa kuwa na Ebola 'haziambatani na ugonjwa huo'.

Mwanamke aliyeshukiwa kuwa na Ebola alitengwa katika Hospitali ya Kericho, eneo la Bonde la Ufa kusini-magharibi mwa Kenya.

"Dalili za mgonjwa haziambatani na ugonjwa wa Ebola ," amewaambia wandishi habari katika uwanja mkuu wa ndege Nairobi alikofanya ukaguzi wa vituo vya udhibiti wa Ebola.

Sampuli za damu za mgonjwa huyo mwenye umri wa miaka 36 zimeonyesha kamba hana virusi vya Ebola.

Mumewe na watu wengine wawili walio karibu naye pia walitengwa.

Maafisa wa afya katika Kaunti ya Kericho wamesema kuwa mwanamke huyo anayekaguliwa alisafiri kutoka Malaba eneo la mpaka kati ya Kenya na Uganda.

Hakuna ripoti yeyote iliyotolewa ya kuwepo kwa ugonjwa wa Ebola karibu na mpaka wa Malaba:Isipokuwa eneo la Magaharibi mwa Uganda.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527