TAKUKURU Yatimiza Agizo la Rais Magufuli....Watumishi Hawa Kuburuzwa Mahakamani

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) leo Jumatatu Juni 10, 2019  imewataja askari polisi wawili na mtumishi mmoja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) waliohusika na ukamataji pamoja na uzuiaji wa mizigo wa mfanyabiashara Ramadhani Ntunzwe.


Takukuru imewataja watumishi hao ni Charity Ngalawa ambaye ni mwajiriwa wa TRA makao makuu, askari Polisi PC Simon Sungu pamoja na askari polisi PC Ramadhani  Uweza wote wakitokea kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi mkuu wa Takukuru, Athuman Diwani imesema watumishi hao wanatuhumiwa kwa kosa la kuomba rushwa ya Sh2 milioni kutoka kwa mfanyabiashara huyo kinyume cha kifungu cha 15(1)(a) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na.11 ya 2007.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post