VIGOGO WA LUCKY VINCENT WATUPWA JELA AJALI ILIYOUA WANAFUNZI 32


Mkurugenzi wa Shule ya Lucky Vincent, Innocent Mushi amehukumiwa kifungo cha miaka 4 au faini ya Sh. Mil. 1.5, huku Makamu Mkuu wa shule, Longino Vicent akihukumiwa mwaka 1 au faini ya Sh. laki 5, kufuatia kukutwa na hatia ya makosa 5 baada ya ajali iliyoua wanafunzi 32.


Hukumu ya kesi hiyo imesomwa leo Jumatatu Juni 10, 2019 na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama, Niku Mwakatobe.



Ajali hiyo, ilitokea Mei 6, 2017, katika eneo la Rhotia wakati, wanafunzi wa shule hiyo, wakitoka Arusha majira ya saa 12 asubuhi kwenda wilayani Karatu, katika mitihani ya ujirani mwema katika Shule ya Tumaini Academy.

Makosa hayo matano ambayo Hakimu Mwakatobe amewakuta na makosa hayo matano ni; kuvunja sheria za usalama barabarani ikiwemo kuendesha gari za abiria bila kuwa na leseni ya usafirishaji, gari lililosababisha ajali kutokuwa na bima, kushindwa kuingia mkataba baina ya dereva na mwajiri na kosa la kuzidisha abiria 13 katika gari lililopata ajali ambalo linamkabili mwalimu mkuu msaidizi.


Hata hivyo, Washtakiwa hao walifanikiwa kulipa faini hiyo na kuachiwa huru.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527