RAIS MAGUFULI AONESHA KUTORIDHISHWA NA UTENDAJI KAZI TPSF

Rais Magufuli amesema licha ya taasisi ya sekta binafsi Tanzania (TPSF) kuwa ya muda mrefu hana uhakika kama inawasaidia wafanyabiashara.


Kiongozi mkuu huyo wa nchi ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Juni 7, 2019 katika mkutano wake na wafanyabiashara kutoka Wilaya zote nchini uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam.

Magufuli amesema kuna ujio wa wafanyabiashara kutoka nje ya nchi lakini hajaona matokeo ya ujio wao tangu waanze kutembelea nchini.

Amesema baadhi ya wafanyabishara wanasema TPSF ni jukwaa la kuwakandamiza  na kuwatengeneza kundi la watu wanaojitiita wawakilishi wakati sivyo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527