MBUNGE ALALAMIKIA KUSHUKA BIASHARA KARIAKOO


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda na Biashara, Seleman Sadiqq, amesema  ukadirio wa kodi unaofanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na kutokuruhusiwa wafanyabiashara wanaonunua bidhaa China na Dubai kwenda na fedha taslimu umekuwa ni tatizo.

Akichangia mjadala wa Bajeti kuu ya Serikali  jana June 18 bungeni Sadiqq alisema tatizo lipo kwenye ukadiriwaji wa kodi na kwamba biashara za Dubai na China zimetawaliwa kwa kulipa fedha taslimu.

“Ni muhimu kwa Benki Kuu (BOT), ueleze utaratibu wa kupeleka fedha taslimu ukoje. BOT wasaidie kuhakikisha biashara inarudi Kariakoo, kwa sasa imepotea katika ramani ya biashara.

“Tulikuwa na Kariakoo ya wafanyabiashara kutoka Malawi, Kariakoo, Burundi, Congo, Uganda na Rwanda, BOT na TRA lazima wajiuelize kuna nini na sababu zipi tulizopoteza biashara Kariakoo,” alisema.

Aidha Mbunge huyo alisema sera ya Tanzania ya viwanda kwa sasa inatekelezeka kwa vitendo kutokana na ujenzi wa viwanda unaofanyika katika maeneo mbalimbali nchini.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527