Angalia Picha : DIAMOND PLATNUMZ ATUA KWA WATOTO WENYE UALBINO SHINYANGA…AWAPA MKONO WA EID-EL-FITR

Msanii Diamond Platnumz ametembelea kituo cha kulelea watoto wenye ualbino Buhangija Mjini Shinyanga na kuwapa zawadi ya sikukuu ya Eid-El-Fitr shilingi 2,000/= kila mmoja huku akikubali ombi la Mkuu wa wilaya ya Shinyanga, Mhe. Jasinta Mboneko la kuweka taa katika kituo hicho ili kuimarisha usalama.

Diamond ametembelea kituo hicho leo Jumanne Juni 4,2019 wakati akitokea Mwanza kwenda Mjini Kahama. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Msanii Diamond Platnumz akisalimiana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga,Geofrey Mwangulumbi.
Diamond Platnumz akiwasalimia kwa kuwapungia mkono watoto wanaolelewa katika Kituo cha Buhangija.
Diamond Platnumz akisalimiana na mtoto Asha
Mtoto Asha akiimba wimbo wa Diamond Platnumz 'Kwangwaru'
Diamond Platnumz akiongea katika kituo cha Buhangija.
Diamond Platnumz akiimba wimbo wa 'Tetema'
Diamond Platnumz akitoa burudani kwa watoto.
Mkuu wa wilaya ya Shinyang,Mhe. Jasinta Mboneko akielezea kuhusu Kituo cha Buhangija na kumuomba Diamond Platnumz asaidie kuweka taa katika kituo hicho ili kuimarisha usalama kwa watoto.
Diamond Platnumz  akitoa zawadi ya shilingi 2000 kwa kila mtoto ikiwa ni zawadi ya sikukuu ya Eid-El-Fitr.
Diamond Platnumz  akitoa zawadi ya shilingi 2000 kwa kila mtoto ikiwa ni zawadi ya sikukuu ya Eid-El-Fitr.
Diamond Platnumz  akitoa zawadi ya shilingi 2000 kwa kila mtoto ikiwa ni zawadi ya sikukuu ya Eid-El-Fitr.
Diamond Platnumz  akiwa na watoto.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post