SHULE ZA SEKONDARI 1241 ZAJENGEWA MABWENI


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa ,na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Seleman Jafo, amesema hadi sasa shule za sekondari 1,241 zimejengewa mabweni kati ya shule za sekondari 3,634 zilizopo kwa kutumia ruzuku kuu.

Jafo amesema hayo leo Jumatatu Mei 27, bungeni jijni Dodoma, wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Azza Hilaly Hamad (CCM).

Katika swali lake, Azza alihoji serikali ina mkakati gani wa kujenga mabweni katika shule za sekondari zilizoanzishwa kitarafa ili kuwasaidia watoto wa kike kupata elimu bora.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527