JAMAA AUA MAMA MJAMZITO,JIRANI NA MAMA MKWE AKIDAI WANAJUA SIRI YA MCHEPUKO


Mtu mmoja ajulikanaye kwa jina la Michael John Mwandu mwenye umri wa miaka 54 mkazi wa Dumila wilaya ya Kilosa amejiua mwenyewe kwa kunywa sumu baada ya kufanya mauaji ya kumuua mke wake Leonola Ernest mwenye miaka 37 akiwa na ujauzito wa miezi kati ya 7 hadi 8.

Tukio hilo limetokea tarehe 24/5/2019 usiku huko Dumila mkoani Morogoro.

Akizungumza na waandishi wa habari Leo Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Morogoro ASCP Wilbrod Mutafungwa amewataja marehemu wengine kuwa ni mama mkwe wa muuaji Magreth Yohana mwenye umri wa miaka 59,Salma Iddi jirani yao mwenye umri wa miaka 52 na pamoja yeye mwenyewe marehemu Michael John ambaye amejiua baada ya kufanya mauaji hayo.

 Chanzo cha vifo hivyo ni wivu wa kimapenzi alioubaini akimtuhumu mke wake kuwa na mahusiano na mwanaume mwingine huku akidai hao wengine walikuwa wakifahamu jambo hilo.

Marehemu ametumia panga kumuua mama yake mkwe huku yeye na marehemu wengine wakinywa sumu aina ya Carbon Furan ambayo ni dawa ya kuua wadudu kwenye mimea
Baadhi ya waandishiwa habari wakimsikiliza Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Morogoro ASCP Wilbrod Mutafungwa wakati akizungumzia mauaji hayo.
Baadhi ya ushahidi ulioonyeshwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro ACP Wilbrod Mutafungwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527