RC MBEYA AWASHUKURU WANANCHI NA VIONGOZI KWA KUFANIKISHA ZIARA YA RAIS MAGUFULI

Ndugu zangu wana Mbeya Tunawashukuru sana wote Kwa umoja wenu na upendo wenu mliouonesha Kwa Mh Rais wetu Dkt John P. Magufuli. 

Mlikuwa wengi na mmefunika. Najua zipo changamoto nyingi ambazo watu wetu waliamua kuandika mabango ili Mh Rais atatue. Nitumie nafasi hii kuwajulisha wote kujenga utamaduni wa kufika ofsn kwangu au kwa wasaidizi wangu maana tumepewa kazi ya kusikiliza na kutatua kero.

Nawashukuru sana CCM Mbeya, Chini ya Uongozi wa Mzee Mwakasole Mwenyekiti, hakika mmetenda haki katika ziara hii. Chama n mshauri na Mwajiri wa Serikali, umoja na mshikamano ndio msingi wa kufika mbele. Nashukuru sana viongozi wa Dini zote Kwa umoja wenu. 

Mmeshikamana na hakika mmetusaidia sana kumsimika Mungu baba katika kila kona ya ziara yetu. Asante sana. Pia nawashukuru sana snaa wafanyabiashara na wadau wengine wote kwa namna mlivyonibeba na kuwa pamoja na mimi katika sherehe za MEI MOSI mmeonesha umoja sana. Assnte sana.

Umefika wakati wa kuijenga Mbeya Kwa kasi na umoja. Sote tuwe na dhamira ya kuifanya Mbeya big city... asante sana sana sana Wana Mbeya, Mbarali, Chunya, Busokelo, Kyela, na kata zake zote.

Mawaziri na Wabunge wote nawashukuru sana. Mh Lukuvi, Mh. Jafo, Mh. Hasunga, Mh. Naibu Speaker, Mh. Biteko, Mh. Kakunda, Mh. Mwanjelwa, Dkt Mwakyembe na Mh Naibu waziri wa ujenzi Pamoja na Mawaziri wengine wote. Wabunge wote wa mkoa huu mmenipa heshima kubwa. Assnte sana Jeshi la Police Kwa kazi nzuri ya kulinda amani chini ya mzee Wangu Kamanda wa Police Mkoa Matei Asante sana

Wakuuu wa Wilaya, Ma DAS na Wakurugenzi wote Ndio mmekuwa kiungo namba Sita katika ziara hii yote. Yote tuliyoagizwa tutatekeleza kama yalivyo. Mmechapa kazi vzr thanks sana.

Asanteni sana snaa. Mimi na wenzangu wote katika ofisi yangu nawashukuru sana

Albert Chalamila
RC Mbeya
03/05/2019


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527