RAIS MAGUFULI AWAONYA WAKURUGENZI WANAOWATOZA USHURU WAKULIMA

Rais John Magufuli amesema ni marufuku kwa wakurugenzi na watendaji wa halmashauri kuwatoza ushuru wasafirishaji wa mazao chini ya tani moja na wafanyabiashara wadogo wenye vitambulisho vya wajasiriamali.

Ametoa onyo hilo  jana Jumanne Aprili 30 katika viwanja vya Mwakangale wilayani Kyela katika ziara yake ya siku nane mkoani Mbeya.

Alisema wapo watendaji wa halmashauri wanaoendelea kutoza ushuru kwa wafanyabiashara hao kwa kudhani kuwa wanapoacha wanapunguza mapato.

“Narudia kwa wakurugenzi na watendaji wote wa halmashauri msiwatoze wananchi ushuru wa mzigo wowote usiozidi tani moja. Mkulima wewe safirisha kutoka hapa peleka mahala popote hakuna wa kukutoza ushuru, na hii sheria imepitishwa na Bunge hayupo yeyote wa kuitengua kwa hivyo mkurugenzi ukitengua umevunja sheria una wajibu wa kufukuzwa kazi.”

“Tuzingatie sheria ya kuwalinda wakulima, pakia viazi, maharage, njugu, chochote ilimradi kisizidi tani moja hakuna kulipia, ukizidisha mie simo,” alisema Rais  Magufuli.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527