BUNGE LA AFRIKA KUSHIRIKIANA NA BUNGE LA UMOJA WA FALME ZA KIARABU( U.AE.)


Makamu wa Rais wa Kwanza wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele akipokelewa na mwenyeji wake,Balozi wa UAE,nchini Afrika Kusini Mahash Saeed Alhameli kabla ya kikao cha majadiliano ya ushirikiano baina ya ujumbe wa Bunge la Afrika na ujumbe kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu (United Arab Emirates- UAE) jana Mei 5,2019 jijini Pretoria,Afrika Kusini.
Kushoto ni Makamu wa Rais wa Kwanza wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele akizungumza tete-a-tete na Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (United Arab Emirates- UAE),nchini Afrika Kusini Mahash Saeed Alhameli.
Makamu wa Rais wa Kwanza wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele akiongoza kikao cha majadiliano kuhusu ushirikiano wa bunge la Afrika na Bunge la Umoja wa Falme za Kiarabu (United Arab Emirates- UAE) ambapo Ujumbe wa Bunge la UAE umeongozwa na Spika wa Bunge la Umoja wa Falme za Kiarabu (United Arab Emirates- UAE), Dk. Amal Abdulla Al Qubaisi ,kwa pamoja wamekubaliana mambo ya msingi ya kushirikiana baina ya mabunge hayo.
Makamu wa Rais wa Kwanza wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele akiagana na mwenyeji wake,Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (United Arab Emirates- UAE),nchini Afrika Kusini Mahash Saeed Alhameli.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post