MAREKANI YATISHIA KUIWEKEA VIKWAZO UTURUKI KUHUSIANA NA MAKOMBORA YA URUSI


Marekani imetishia kuiwekea vikwazo Uturuki endapo haitoacha kununua mfumo wa ulinzi wa makombora wa S-400 kutoka Urusi.

 Uturuki inakusudia kulilinda anga lake kwa kutumia mfumo huo wa ulinzi uliotengenezwa Urusi, lakini maafisa mjini Washington wanaitaka Uturuki ambayo ni mshirika wake katika ya Jumuiya ya kujihami NATO kununua mfumo kama huo wa ulinzi uliotengenezwa Marekani. 

Kwa mujibu wa kituo cha utangazaji cha CNBC, serikali ya Marekani imeipatia Uturuki muda wa wiki mbili kuachana na mfumo kutoka Urusi la sivyo itakabiliwa na vikwazo ikiwa ni pamoja na kuacha kuiuzia ndege za kivita za F-35. 

Hata hivyo mapema wiki hii waziri wa ulinzi wa Uturuki Hulusi Akar alisema vikosi vyake tayari vinapokea mafunzo ya kutumia mfumo wa S-400 nchini Urusi na kuwa mfumo huo ulitarajiwa kuwasili nchini Uturuki mwezi Juni au Julai.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post