MAKAMBA ASISITIZA JUNI MOSI NDO MWISHO WA MATUMIZI YA MIFUKO YA PLASTIKI


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba amesema kuanzia Juni Mosi mwaka huu itakuwa ndio mwisho wa matumizi ya mifuko ya plastiki na Sheria kali zitachukuliwa kwa yeyote atakayekiuka maagizo hayo.

Amesema hayo Mei 22 Jijini Dar es Salaam, kwenye kikao cha viongozi na watendaji mkoani hapo kilichokuwa kinahusu marufuku ya matumizi ya mifuko ya plastiki.

Makamba Amesema, ofisi yake kwa kushirikiana na ofisi ya Tamisemi watapita kwenye maduka na Magenge kwa ajili ya kukagua na kuangalia kama agizo linatekelezwa.

“Wazalishaji wa mifuko hiyo wakibainishwa bado wanazalisha faini itakuwa shilingi milioni 20 na kifungo, waingizaji katoka nje nao faini milioni 20, huku mtumiaji faini yake ikiwa ni 30,000.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527