MWENYE JINSIA MBILI AGOMA KUNYOA NYWELE

Alok Vaid-Menon ni mshairi na mwana harakati wa kutetea wanamitindo waliozaliwa na jinsia mbili (kiume na kike) katika mitandao ya kijamii. Lakini mara nyingi watu hukemjeli.

Mara ya kwanza alipoifahamisha familia yake kuwa ana jinsia mbili na kwamba angelipendelea kuangazia zaidi jinsia ya kike, swali la kwanza lilikua , "Lakini una nywele nyingi sana mwilini! Utapata tabu sana kuzitoa zote ili upate muonekano wa kike, kwa hivyo achana na wazo hilo."

Familia yake iliangazia zaidi nywele nyingi alizokuwa nazo mwilini kiasi cha kumzuia kujitambulisha kwa umma kama mwanamke.

''Watu bado wana uelewa mdogioo kuhusu masuala ya watu waliyozaliwa na jinsia mbili'' alisema Alok Menon.

Jamii imetawaliwa na dhana ya kuwa watu waliozaliwa na jinsia mbili ima wanataka kuwa mwanamume au mwanamke lakini haijawahi kutathmini mahitaji mingine ya watu hao linapokuja suala la jinsi wao wanavyotaka kutambulisha jinsia yao kwa hadharani.

Alipoamua kuangazia jinsia yake ya kike zaidi japo muonekano wake ni wa kiume alijiunga na kikundi cha watu waliyozaliwa na jinsia mbili kama yeye ili kubadilishana mawazo na pia kupeana motisha kuhusu hali wanazokumbana nazo katika jamii.

''Nimekuwa nikibadilisha mavazi yangu kulingana na hisia zangu wakati mwingine navaa mavazi ya kiume na mara nyingine navalia mavai ya kike, hali hiyo ilikuwa ikiwakanganya watu sana'' alisema.

Kwa mfano akivalia rinda, wanawake walikuwa wakimchukulia kama mwanamke mwenzao na umuliza kwa mshangao "Alaa, sasa umekuwa mwenzetu?"
Baadhi ya wenzake katika kikundi alichojiunga nacho walimwambia, ni vyema achague moja kati ya jinsia hizo mbili.
"Ikiwa unataka watu wabadili msimamo wao kukuhusu kama mtu aliyezaliwa na jinsia mbili basi unahitaji kunyoa nywele zote mwilini na kutafuta ushauri wa kitaalamuli upete matibabu itakayokusaidia kusalia na jinsia moja."

Lakini wazo hilo lilimkera sana kwasabau tayari alikuwaakipata ushauri kutoka kwa kila mtu kuhusu maisha yake. Anasema alijiunga na kundi hilo ikidhani kuwa wenzake wataheshimu uamuzi wake.

''Bado kuna dhana kuhusu urembo ambayo ni kigezo kinachoongoza jinsia ya kike - kwamba haiwezekani uwe mwanamke ukiwa na nywele kila mahali mwilini'', alisema Menon.

Hata hivyo bado anakabiliana na changamoto ya kujieleza yeye ni nani huku wale wanaomuelewa hasa katika mitandao ya kijamii wakimshauri aachane na juhudi za kutafuta muonekano wa kuwa mwanamke.

Wanafanya hivyo kwa kumjali lakini anasema kuwa yeye hujiuliza maswali mengi sana kama vile "Wananitakia nini wakati ni uamuzi wa kibinafsi?"

Mara ya kwanza alipogundua kuwa anastahili kuchukia nywele na nyingi mwilini alikuwa na miaka 10.

Dada yake mkubwaa mbaye wakati huo alikuwa na miaka 13 alikuwa na nywele kidogo tu zilizomea makwapani.

''Nywele zangu zilipoanza kumea zilinijaa kila sehemu mwilini'', alisema Menon.

Anaongeza kuwa alishangazwa na jinsi kila mtu katika familia yake alivyokuwa akijitolea kumnyoa.

Ni hapo alianza kuwa kujiuliza maswali kuhusu nywele zake na alipouliza maswali zaidi alifahamishwa kuwa zilitokana na maumbile yake.
Nywele ziliendelea kumea kadri alivyokua mkubwa na alihisi uchungu wakati wa kunyolewa hadi baba yake akaamua kuwa asinyolewe tena kutokana na matatizo aliyokuwa akipata.

''Nilimraia baba aniruhusu kunyoa nywele zangu mwilini lakini alikataa kabisa''

Watoto shuleni walikuwa wakimkejeli kwa kuwa na nywele nyingi mwilini, huku wengine wakimfananisha na "mnyama" au uchafu.

Alipofikisha miaka 11, kejeli kutoka kwa watu zilizidi kiasi cha wengine kuitenga familia yake wakidai ni ''magaidi''

Alikuwa akiishi na jamaa zake katika mji mmoja jimboni Texas Marekani katika moha ya maeneo yaliokuwa na jamii ya wahindi waliokuwa wachache.

Watu walianza kuwaita magaidi na wakati kuna mmoja mtu alimuuliza, "Kwanini watu wako wamekufanyia hivi?"

Alipofikisha umri wa miaka 13 hatimae baba yake alimruhusu kunyoa nywele zake mwilini.

''Nakumbuka hiyo siku, nilijihisi vizuri sana kwasababu sasa nitafanana na wasichana wenzangu darasani'', alisema.

''Kwa kweli hatua hiyo ilinisaidia kwasababu kejeli zao zilipungua.''

Alipojiunga na shule ya upili hali ilibadilika kabisa kwani wanafunzi wenzake walishangazwa na uwezo wake wa kufuga ndevu hadi zikawa kubwa kiasi hicho.

''Hata nilijiunga na kundi lililojiita ''ndevu za amani''ambapo tulikua tukijadili masuala kama kujiepusha na ghasia na vurugu shuleni- Nakumbuka nilipewa tuzo kutokana na ndevu zangu nyingi.''

Hatua hiyo ilimfanya ajipende na kujithamini zaidi na ni hapo anasema ''Niliamua kufanya maamuzi yangu mwenyewe kuhusu muonekano unaoniridhisha''
Anasema kuwa na nywele nyingi mwilini hakustahili kuhusishwa na jinsia ya mtu kwasababu kila mtu ana kiwango fulani cha nywele mwilini mwake.

''Sioni kwanini kitu ambacho kinatokana na maumbile yamtu kinaweza kuwafanya watu kumhukumu muathiriwa''

Menon anasema watu wanaofanya biashara ya kuuza wembe na krimu za kuondoa mwele mwili hawangelipata umaarufu kama kila mtu angelizipenda nywele zake mwilini.

''Napenda kuchezea nywele zangu za mwilini kwasababu zinaniliwaza, wakakati mwingine nahisi kana kwamba ni blanketi inayoniongezea joto mwilini''

Anaongezea kusema kuwa anapendelea kuona nywele zake zikichomoza nje ya nguo yake ''Nazichukulia kama sehemu ya urembo wangu'' alisema.

Lakini suala la kufuga nywele kwa watu waliozaliwa na jinsia mbili lina madhara makubwa kama vile kunyanyaswa na watu.

Wataalau wa tiba kwa watu hao wanasema kufanya hivyo ni kuhatarisha maishakwani popote wanapoenda wanavutia hisia za watu ambao wakati mwingine hufikiria wao ni wapenzi wa jinsia moja.

Suala la kutaka kujionesha ndio linachangi wao kuvamiwa hadharani na kutusiwa mitabndaoni kila siku.

Utafiti unaonesha watu waliozaliwa na jinsia mbili wanakabiliwa na msongo mkubwa wa mawazo kutokana na kejeli zawatu wengine katika jamii.

Alok Menon anasema Pengine maisha yangekuwa tofauti kama ningelinyoa,lakini kwanini iwe hivyo?'

Kuwa na nywele mwilini anasema ni sehemu ya maumbile yake na kwamba ni uamuzi wa kibinafsi wa kuuambia ulimwengu, "Niko hapa kuishi!"

Picha za zimepigwa na Brian Vu.

Chanzo- BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527