GWAJIMA KUONGEA NA VYOMBO VYA HABARI LEO SAA TANO

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima leo Jumatano Mei 8, 2019 anatarajiwa kuzungumza na waandishi wa habari kanisani kwake Ubungo Jijini Dar es Salaam ikiwa ni siku moja baada ya kuhusishwa na video ya ngono.

Taarifa hiyo imekuja kufuatia kusambaa kwa video ikimuonyesha mtu anayedhaniwa ni yeye akiwa faragha na mwanamke wakifanya mapenzi.

Jana baada ya kusambaa kwa video hiyo Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa alinukuliwa akisema tayari wameshamwita Gwajima kwa ajili ya kutoa maelezo kuhusu video hiyo.

“Tayari askofu Gwajima ameitwa polisi kwa ajili ya kuhojiwa na ataripoti kesho (leo) asubuhi , akichelewa atakamatwa na tumemuita sababu hakuna aliyelalamika lakini tumeona ni kitendo cha ukiukwaji wa maadili, awe askofu awe mtu wa kawaida ule ni unyama, “alisema Mambosasa


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527