BOBI WINE, BESIGYE WATENGENEZA JEMBE MOJA LA KUMLIMIA MUSEVENI


Mbunge wa upinzani nchini Uganda ambaye pia ni msanii wa muziki, Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine, ameungana na mwanaharakati wa kisiasa Dkt. Kizza Besigye ili kukiondoa madarakani chama tawala cha National Resistance Movement (NRM) kinachoongozwa na Rais Yoweri Museveni.

Taarifa iliyotolewa na wapinzani hao wenye nguvu zaidi nchini Uganda, imeeleza kuwa baada ya mazungumzo kati yao, wamekubaliana kuhusu masuala kadhaa ya kushirikiana kisiasa dhidi ya Museveni kwenye uchaguzi mkuu ujao mwaka 2021.

Akizungumza na waandishi habari jana, Bobi Wine alisema wamekuwa wakishauriana katika mikutano kadhaa na vyama tofuati vya kisiasa nchini kikiwemo cha Democratic Party maarufu DP na kiongozi wa People’s Government, Dkt. Kizza Besigye.

Bobi ambaye hana chama, ni mgombea huru na kwa sasa ni Mbunge wa Jimbo la Kyadondo,

NRM kimekuwa madarakani tangu 1986.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527