RAIS WA ALGERIA BOUTEFLIKA ATANGAZA KUJIUZULU


Rais wa Algeria Bouteflika (82) ambae anatumia wheelchair kutembelea amejiuzulu wadhifa wake baada ya kukaa madarakani kwa miaka 20, hatua hiyo inakuja baada ya Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Algeria Ahmed Gaid Salah kumtaka Rais huyo ajiuzulu haraka iwezekanavyo.

Kulikuwa na shangwe na vifijo kwenye mji mkuu Algiers baada ya kutangazwa uamuzi huo jana usiku. Televisheni ya taifa ilitangaza kuwa Bouteflika alilishauri rasmi Baraza la Katiba kuwa anaachia madaraka kama Rais wa Algeria. 

Alisema uamuzi huo uliochukuliwa kwa dhati unalenga kuchangia katika kuituliza mioyo na fikra za Waalgeria, na kuwawezesha kuiongoza Algeria kuwa na mustakabali mzuri na ambao wana haki ya kuufanikisha. 

Video ilimuonyesha Bouteflika, akiwa kwenye kiti cha walemavu, akikabidhi barua yake ya kujiuzulu kwa mkuu wa Baraza la Kikatiba Tayeb Belaiz.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527